“WAZIRI wa Usalama wa Ndani Kipchumba Murkomen ametangaza mpango wa kupeleka kikosi maalum cha polisi katika Bonde la Kerio ili kuimarisha msako dhidi ya utengenezaji na matumizi ya pombe haramu. Waziri Murkomen vilevile ameonya kuwa afisa wa utawala wa eneo hilo anayeshukiwa kuhimiza ulevi atachukuliwa hatua za kinidhamu. Akizungumza akiwa Metkei, Keiyo Kusini, Murkomen alionya hatua kali dhidi ya maafisa wa serikali ya kitaifa na usalama wanaoshirikiana au kuzilinda biashara za pombe haramu. “Serikali haitalegeza msimamo wake katika vita dhidi ya pombe haramu, hata kama itabidi kupeleka kikosi maalum kuwasaka wahusika,” alisema.
Original story
Continue reading at Taifa Leo (Swahili)
taifaleo.nation.co.ke
Summary generated from the RSS feed of Taifa Leo (Swahili). All article rights belong to the original publisher. Click through to read the full piece on taifaleo.nation.co.ke.
