“LICHA ya kaunti ya Taita Taveta kuahidiwa na Rais William Ruto kuwa itapokea asilima 50 ya mapato ya Tsavo miaka mitatu iliyopita, bado ahadi hiyo haijatekelezwa huku Gavana Andrew Mwadime akiomba Bunge la Taifa kutekeleza amri hiyo. Gavana Mwadime alipendekeza sehemu ya Tsavo ibadilishwe kuwa hifadhi ya kitaifa, kuwe na usimamizi wa pamoja na pia mfumo wa mgawanyo wa mapato. “Zaidi ya kilomita za mraba 10,650 za ardhi ya kaunti zimetengwa kwa ajili ya hifadhi hizo, hali inayowaacha wakazi na sehemu ndogo ya kuishi, kulima na kuendesha shughuli za kiuchumi, licha ya kaunti kubeba mzigo wa migogoro kati ya binadamu na wanyamapori ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mazao, mifugo na hata vifo,” alisema Bw Mwadime. Ombi hilo linatokana na wasilisho la umma kutoka kwa aliyekuwa Spika wa Bunge la Kaunti, Bw Anselim Mwadime, likilenga kuruhusu usimamizi wa pamoja na mgao wa mapato. Kamati ya Maombi ya Umma sasa inatarajiwa kuchambua hoja hiyo kabla ya kuwasilisha ripoti na mapendekezo yake kwa Bunge la Kitaifa.
Original story
Continue reading at Taifa Leo (Swahili)
taifaleo.nation.co.ke
Summary generated from the RSS feed of Taifa Leo (Swahili). All article rights belong to the original publisher. Click through to read the full piece on taifaleo.nation.co.ke.
