skipToContent
All countries
Country

Kenya

894 stories

Taifa Leo (Swahili)

Makala ya mwaka huu ya Safaricom Chapa Dimba yazinduliwa

MAKALA ya tano ya michuano ya Safaricom Chapa Dimba, yalizinduliwa rasmi Jumamosi katika Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, Kisumu. Katika msimu huu mpya, wachezaji bora 32 watakaochaguliwa kutoka mashindanoni ya mwaka huu watapata nafasi ya kuiwakilisha Kenya kwenye dimba la Kombe la Gothia nchini Uswidi. Mbali na michezo, Safaricom imeweka mkazo mkubwa kwenye elimu ambapo vijana 150 bora watanufaika na ufadhili wa masomo ya juu kupitia mpango wa Citizens of the Future. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Safaricom PLC Peter Ndegwa alisema kampuni hiyo inalenga kutumia michezo, elimu na teknolojia kubadilisha maisha ya vijana nchini. “Tunataka kukuza si tu wanasoka bora, bali vijana waliokomaa na wenye uwezo wa kuleta mabadiliko nchini,” alisema Ndegwa ambaye aliandamana na viongozi wa Shirikisho la Soka nchini (FKF) akiwemo ras wa shirikisho hilo Hussein Mohammed. Katika mabadiliko mapya, waandalizi wamepunguza umri wa washiriki kutoka miaka 16-20 hadi 15-18 ili kuwezesha vipaji kugunduliwa mapema na kupata nafasi katika soka ya kulipwa nchini na kimataifa. Safaricom pia imeongeza matumizi ya teknolojia katika usajili na uchambuzi wa wachezaji. Baada ya mafanikio ya matumizi ya vifaa vya AI na GPS msimu uliopita, safari hii kampuni hiyo italeta kamera za VeO pamoja na vifaa vya MyScout AI kuanzia ngazi ya kaunti. Teknolojia hiyo itasaidia kufuatilia wachezaji, kasi, nafasi wanazocheza na kiwango chao cha mchezo huku ikiwajengea wasifu wa kidijitali utakaoweza kuonekana na maskauti wa kimataifa. Mashindano hayo yatafanyika katika maeneo manane nchini katika ngazi ya wadi, kaunti, mikoa na fainali ya kitaifa. Usajili wa timu za wavulana na wasichana umefunguliwa kupitia tovuti ya Safaricom Chapa Dimba Washindi wa kitaifa katika kila kundi watajinyakulia Sh1 milioni huku zawadi nyingine zikitolewa katika ngazi za kaunti na mikoa pamoja na tuzo za mfungaji bora, kipa bora na mchezaji bora. Tangu kuanzishwa mwaka 2017, mashindano hayo yamelea mastaa kadhaa wanaocheza soka ya kulipwa akiwemo Benson Omalla, Bryton Otieno, Austine Odongo, Derrick Oketch, Jentrix Shikangwa, Marion Serenge na Mercy Akoth. Baadhi ya nyota hao pia wameiwakilisha Kenya katika mashindano ya kimataifa yakiwemo Kombe la Dunia la Mabinti la wachezaji chini ya miaka 17. Mashindano hayo yanaandaliwa kwa ushirikiano na FKF kama sehemu ya juhudi za kukuza soka ya vijana mashinani nchini Kenya.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Kenya Police Bullets mabingwa KWPL

Kenya Police Bullets ndio mabingwa wa Ligi kuu ya Wanawake (KWPL) msimu huyu wa 2025/26. Bullets ya kocha David Bujego, imechukua ubingwa huo mara tatu mtawalia sasa (2023/24 na 2025/25 wakati huo ikinolewa na Beldine Odemba ambaye aliondoka mwishoni mwa msimu jana). Washikadoria hao walijihakikishia ubingwa, baada ya ushindi finyu wa 1-0 dhidi ya Trinity Starlets jana, katika uwanja wa Trinity Complex mjini Gilgil Kaunti ya Nakuru leo. Bao hilo la pekee lilifungwa na mshambuliaji raia wa Uganda Margaret Kunihira dakika ya 40 ya mchezo. Bao hilo lilikuwa la 14 la Kunihira msimu huu, akiwa anaongoza jedwali la wafungaji bora kutoka na mechi 19. Bullets sasa itawakilisha Kenya katika michuano ya Baraza la Mashirikisho ya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ya kufuzu michuano ya klabu bingwa Afrika nchini Rwanda baadae mwaka huu. Mara ya kwanza Bullets walishiriki 2024 nchini Ethiopia na wakamaliza nafasi ya pili mwaka jana walimaliza wa tatu katika mashindano yaliyoandaliwa jijini Nairobi. Ikiwa imesalia mechi moja msimu kukamilika wikendi hii, Bullets wanaongoza jedwali kwa alama 49. Starlets kwa upande mwingine walidondoka hadi nafasi ya tano wakiwa na alama 33. Katika mechi nyingine, Kibera Soccer Women walimaliza msimu nafasi ya tatu kwa alama 34 baada ya ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Zetecg Sparks. Mabao hayo yalifungwa na Neema Dorcas (2), Amina Nyakoa (32) na Ann Arusi (38). Mvua ya mabao ilishudiwa katika uwanja wa Mumboha Kaunti ya Vihiga ambapo, mabingwa wa zamani Vihiga Queens walipata ushindi wa 3-0 dhidi ya Gideon Starlets. Soccer Assassins nao walilala mikononi mwa Kayole Starlets ambao waliwapiga 1-0. Matokeo ya Jumapili Trinity Starlets 0-1 Kenya Police Bullets Zetech Sparks 0-3 Kibera Soccer Women Soccer Assassins 0-1 Kayole Starlets Vihiga Queens 3-2 Gideon Starlets

10 May 2026

Daily Nation Kenya

A 12-year land case, a counter claim collapses as court rules both sides failed to prove ownership

Court rules that neither side met the legal threshold required in the case.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

African lobby groups’ wish list ahead of Africa Forward Summit

More than 30 heads of state are expected to attend the two-day event.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Jinsi DCP ilifaulu kupata idadi kubwa ya wapigakura mchujo wa Ol Kalou

Mshindi katika mchujo wa DCP Sammy Ngotho alijipatia kura 12,957 ikilinganishwa na mshindi wa UDA Samuel Muchina aliyepata kura 3,221.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Nganya graffiti ban: Matatu industry plans Court of Appeal, Parliament fightback

Stakeholders warn that strict enforcement of transport rules risks wiping out jobs.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Form Four students miss out on learning at Jamhuri High School following plastic seats standoff

Parents maintain the 27 students did not destroy any school property.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Bilionea Aliko Dangote awazia kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta Kenya

BILIONEA wa Nigeria Aliko Dangote anatathmini kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta chenye uwezo wa kuchakata mapipa 650,000 kwa siku hapa nchini. Kulingana na taarifa ya gazeti la Financial Times iliyochapishwa Jumapili, bwenyenye huyo analenga kufanya hivyo ili kuinua uchumi wa Afrika Mashariki. “Nalenga zaidi Mombasa kwa sababu ina bandari kubwa zaidi na yenye kina kirefu,” akasema Dangote katika mahojiano na FT. Taarifa hiyo inatokea mwezi mmoja baada ya Rais William Ruto kusema kuwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zilikuwa kwenye mazungumzo kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha pamoja cha kusafisha mafuta katika Bandari ya Tanga, Tanzania. Kiwanda anacholenga Dangote kitakuwa sawa na kile ambacho amekijenga kwao Nigeria. Akilinganisha bandari ya Mombasa na ile ya Tanga, Dangote alipendelea Kenya akisema ni pazuri zaidi kutokana na ukubwa wa uchumi wake na kiwango cha juu cha matumizi ya bidhaa za mafuta. “Wakenya hutumia mafuta zaidi na uchumi wake ni mkubwa zaidi,” akasema. Ingawa hivyo, tajiri huyo alisema kuwa hatua itakayofuata sasa iko mikononi mwa Rais Ruto. “Mwelekeo sasa utatoka kwa Rais Ruto. Chochote ambacho Rais Ruto atasema ndicho nitakachofanya,” alisema akisisitiza ushirikiano lazima utoke kwa nchi za EAC. Kulingana na taarifa za Financial Times, Dangote anakadiria kuwa itagharimu kati ya dola bilioni 15 (Sh1.9 trilioni) hadi 17 (Sh2.1 trilioni) kujenga kiwanda hicho cha kusafisha mafuta. Kwa sasa, nchi za Afrika Mashariki huagiza bidhaa zote za mafuta yaliyosafishwa kutoka nje, hasa kutoka Mashariki ya Kati. Nchi za EAC ni kati ya zile zilizokumbwa na uhaba wa mafuta wakati vita vilikuwa vikiendelea kati ya Amerika-Israel dhidi ya Iran.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

How perceived frontrunner Wambugu Kanuria lost Ol Kalou UDA nominations to ex-MP aide

Miscalculations that cost UDA man party ticket in Ol Kalou nominations.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Swiss firm sued for using ‘harmful’ fuel markers in Kenyan market

Cofek accuses SICPA of using chemical markers containing halogen-based elements at higher levels.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Why Garissa flood victims refused to leave the danger zone

Victims justify their decision to stay in flood-prone areas.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Ngong Racecourse hosts one of Kenya’s classic races, the Kenya Oaks

The Kenya Oaks has attracted a field of seven runners who will battle it out over a distance of...

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Divide or unite Mt Kenya? The tough choices facing Ndindi Nyoro as politicians woo him

Major political heavyweights are openly competing to recruit Ndindi.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Pensheni: Vitisho baridi dhidi ya Uhuru

KAULI za baadhi ya viongozi wa Kenya Kwanza kutaka marupurupu ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta yapunguzwe au yaondolewe zimeendelea kuzua mjadala mkali, huku wakosoaji wakionya dhidi ya kutumia sheria kama silaha ya kisiasa. Seneta wa Nandi Samson Cherargei, ambaye ni mshirika wa Rais William Ruto, alipendekeza Uhuru apokonywe marupurupu hayo kwa kuendelea kushiriki siasa kinyume cha sheria baada ya kustaafu. Hata hivyo, pendekezo hilo lilipuuzwa na wandani wa Rais Ruto pamoja na wataalamu wa Katiba wakisema ni siasa za pesa nane. Mbunge wa Belgut Nelson Koech, ambaye ni mwandani wa karibu wa kiongozi wa nchi, alimtetea Uhuru, akisema viongozi wanapaswa kuheshimu Katiba na haki zinazotolewa kwa marais wastaafu. Akizungumza katika mazishi kijijini Chemororoch, Kaunti ya Kericho, Koech alipinga vikali mjadala kuhusu kuondolewa kwa marupurupu ya rais huyo wa nne wa Kenya. “Wachana na hii mambo kidogo kidogo, mambo ambayo haisaidii. Kumwandama Uhuru Kenyatta, kwa nini tufanye hivyo. Sasa marupurupu ya mtu ambayo yako kwa katiba unasemaje yatatolewa?” akahoji. Alisisitiza kuwa marupurupu ya rais mstaafu yamelindwa kikatiba na hayapaswi kutumiwa kama njia ya kulipiza kisasi cha kisiasa viongozi wanapotofautiana. Koech pia aliwataka viongozi kuwa waadilifu na kuwatendea wengine jinsi wanavyotaka kutendewa siku zijazo watakapostaafu mamlakani. “Tuwatendee wengine tunavyotaka kutendewa pia. Wacha Uhuru aende na zake,” alisema. Kauli zake zilijiri wakati ambapo baadhi ya viongozi wa kisiasa wamekuwa wakitaka marupurupu ya marais wastaafu yapitiwe upya, hasa kufuatia mvutano wa kisiasa kati ya Uhuru na utawala wa Kenya Kwanza. Cherargei amepeleka hoja Seneti akitaka marupurupu ya Uhuru yasitishwe au yapunguzwe. Alisema rais huyo mstaafu hawezi kuendelea kufaidika na fedha za umma huku akiendelea kushiriki siasa kama kiongozi wa chama cha Jubilee. Katika hoja yake, Cherargei anataka fedha zitakazookolewa kutokana na kupunguzwa kwa marupurupu hayo zielekezwe kwa maendeleo ya wananchi. Lakini hoja hiyo imepingwa vikali na baadhi ya viongozi wa upinzani na hata baadhi ya wabunge wanaounga serikali. Mbunge wa Rarieda Otiende Amollo alisema mjadala huo ni “kupoteza muda,” akieleza kuwa Katiba inalinda marupurupu ya rais mstaafu chini ya Kifungu cha 151(3). “Mijadala mingine ni kupoteza muda. Hoja hii ya Seneta Cherargei haina msingi. Marupurupu ya rais mstaafu hayawezi kubadilishwa akiwa hai. Tulihakikisha hilo linawekwa kwenye Katiba.” Mvutano huo uliongezeka baada ya Uhuru kutoa hotuba kupitia simu ya ndugu yake Muhoho Kenyatta, ambapo alimshutumu Rais Ruto kwa kujaribu kumzima kisiasa. Uhuru alisema ana haki ya kutetea chama chake kama wafanyavyo viongozi wengine wa dunia hata baada ya kustaafu. Rais huyo mstaafu aliapa kuwa hatafumbwa mdomo na yeyote. Wadadisi wa siasa wanahoji kwamba hatua ya Cherargei ni baridi sana japo wanasisitiza katika siasa hakuna la kupuuzwa. “Hata kiti cha naibu rais kilionekana kuwa kimelindwa katika katiba hadi alipotofautiana na rais na akaondolewa. Hata hivyo, vitisho vya kuvua Uhuru posho lake kama rais mstaafu ni baridi,” asema mchanganuzi Peter Katana.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Why unhealed leaders wound their nations

When unresolved trauma meets power and authority, fear often becomes policy.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Green power: A France-Kenya partnership for clean energy

In France, thanks to nuclear and renewables, 95 per cent of electricity generation is...

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Africa’s role in global green industrialisation

For decades, Africa’s role in the global economy was defined by the extraction and exportation...

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Unafahamu kuwa chakula na maji unayokunywa yanatokana na nyuki?

KATIKA kipindi hiki cha mabadiliko ya tabianchi, uzalishaji wa chakula duniani unazidi kuwa kwenye njiapanda na hatarini. Lakini mbali na ukame, mvua zisizotabirika na gharama ya uzalishaji kupanda, kuna tishio jingine ambalo wengi hulipuuza—kutoweka kwa nyuki. Wadudu hawa wadogo wana mchango mkubwa mno katika uzalishaji wa chakula kuliko wengi wanavyofahamu. Bila nyuki, mazao mengi yasingeweza kuzaa kwa kiwango kinachohitajika, ubora wa matunda na mboga ungeshuka, huku mifumo ya kilimo ikiathirika. Nyuki ndio wachavushaji wakuu wa mimea (pollinators). Kupitia uchavushaji mtambuka (cross pollination), wanahakikisha maua yanageuka kuwa matunda, mbegu na mazao yenye tija. Pia, husaidia uchavushaji mtambuka wa mimea, jambo linaloongeza uzalishaji na kuboresha ubora wa mazao mashambani. Kulingana na Dkt Monica Olala, Mkuu wa Maendeleo ya Raslimali za Wanyama chini ya Idara ya Maendeleo ya Mifugo inayosimamia pia ufugaji nyuki, mchango wa nyuki haupaswi kupimwa kwa asali pekee. “Watu wengi bado wanaamini nyuki yupo kwa ajili ya asali pekee, lakini ukweli ni kwamba mchango wao mkubwa uko katika uchavushaji wa mazao. Bila nyuki, uzalishaji wa chakula ungeathirika pakubwa,” anasema. [caption id="attachment_187899" align="aligncenter" width="300"] Dkt Monica Olala, Mkuu wa Maendeleo ya Raslimali za Wanyama chini ya Idara ya Maendeleo ya Mifugo inayosimamia pia ufugaji nyuki, wakati wa mahojiano Jijini Nairobi. Picha|Sammy Waweru [/caption] Anafafanua kuwa karibu asilimia 75 ya mazao yanayolimwa hutegemea uchavushaji wa nyuki kwa kiwango fulani. Hivyo, kulinda nyuki ni sawa na kulinda uzalishaji wa chakula na uchumi wa kilimo. “Tukiwekeza zaidi katika ufugaji nyuki na utunzaji wa mazingira yao, tutaimarisha sekta nzima ya kilimo,” anaongeza. Mbali na mazao ya chakula, nyuki pia wana mchango mkubwa katika uzalishaji wa malisho ya mifugo. Dkt Olala anasema nyuki huchavusha mimea inayotumika kama chakula cha mifugo, jambo linaloongeza upatikanaji wa malisho bora. “Kenya kwa sasa inakidhi takribani asilimia 40 pekee ya mahitaji ya malisho ya mifugo. Pengo lililopo linaathiri wafugaji wa ng’ombe wa maziwa, nyama na kuku. Uchavushaji bora kupitia nyuki unaweza kusaidia kuongeza uzalishaji wa malisho,” anasema. Licha ya umuhimu huo mkubwa, sekta ya ufugaji nyuki nchini bado inakabiliwa na changamoto nyingi. Takwimu za mwaka 2024 kutoka Wizara ya Kilimo na Maendeleo ya Mifugo zinaonyesha kuwa Kenya huzalisha karibu tani 19,000 za asali kwa mwaka, kiwango kilichoshuka kutoka tani 35,000 zilizokuwa zikizalishwa hapo awali. Kuporomoka huku kwa uzalishaji wa asali kunahusishwa na mabadiliko ya tabianchi, matumizi holela ya dawa za kemikali mashambani na uvamizi wa nzige ulioshuhudiwa kati ya mwaka 2019 na 2021. [caption id="attachment_187900" align="aligncenter" width="300"] Nyuki ni mdudu muhimu sana katika uzalishaji wa asali. Picha|Sammy Waweru [/caption] “Kipindi kirefu cha ukame, mvua zisizotabirika na uharibifu wa mazingira hupunguza mimea ya maua ambayo ni chanzo cha chakula kwa nyuki. Aidha, matumizi ya dawa za kemikali yameharibu makundi mengi ya nyuki,” anaeleza. Anakumbusha taifa kuwa kuwa wakati wa operesheni za kudhibiti nzige katika baadhi ya maeneo, makazi ya nyuki na mizinga mingi iliathirika vibaya, huku baadhi ya maeneo yakipoteza hadi asilimia 50 ya nyuki. Kwa wakulima, ujumbe wake ni wazi: hata kama hawafugi nyuki, bado wanawahitaji. “Bila uchavushaji, mavuno hupungua na ubora wa mazao hushuka. Nyuki ni sehemu muhimu ya mfumo wa uzalishaji wa chakula na uchumi wa kilimo,” anasema. Isitoshe, Dkt Olala anasema maadhimisho ya kimataifa ya Siku ya Nyuki Duniani, yaani World Bee Day ambayo huadhimishwa kila Mei 20, ni jukwaa muhimu kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa kutunza nyuki na kuhifadhi mazingira yao. [caption id="attachment_187901" align="aligncenter" width="300"] Wafugaji wa nyuki katika Kaunti ya Nyeri wakiwa kwenye jengo maalum la nyuki - apiary. Picha|Sammy Waweru [/caption] Anadokeza kwamba maadhimisho ya mwaka huu, 2026, yatafanyika Mama Ngina Drive, Mombasa, yakilenga kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo pamoja na kuonyesha bidhaa zitokanazo na nyuki. “Madhumuni ni kuhamasisha jamii kuelewa kuwa nyuki si wadudu wa kawaida. Ni msingi muhimu wa uzalishaji wa chakula, lishe na uchumi,” anasema. Aidha, Kenya imepanga kuandaa mbio za nyika za kimataifa mwaka 2027 kama sehemu ya kampeni ya kuhamasisha uhifadhi wa nyuki na mazingira yao. Kadri dunia inavyokabiliwa na changamoto za usalama wa chakula na mabadiliko ya tabianchi, wataalamu wanaonya kuwa kulinda nyuki si hiari tena, bali ni jukumu la pamoja kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Zena Ibrahim: Sky the limit for chess prodigy

Talented 17-year-old Sironga Girls High School student flying Kenya's flag high

10 May 2026

Daily Nation Kenya

'Family values' are leaving too many families behind

Families on the margins are forced to absorb economic and social gaps.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Ruto, Gachagua, wang’ang’ania Nyoro 2027 ukikaribia

MBUNGE wa Kiharu Ndindi Nyoro amejikuta katikati ya mvutano mkali wa kisiasa Mlima Kenya, ambapo mirengo mikuu ya kisiasa inammezea mate kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2027. Baada ya kujijenga kwa takriban miaka 10, Nyoro sasa ameibuka kuwa kigogo katika siasa za eneo hilo. Rais William Ruto, kiongozi wa Democracy for Citizens Party Rigathi Gachagua, Fred Matiang’i na Babu Owino wote wanamng’ang’ania kisiasa. Rais Ruto amemwita Nyoro “mwanafunzi wake wa kisiasa”, akionyesha uwezekano wa kushirikiana naye. Matiang’i naye amedai kushirikiana naye kwa karibu, huku Gachagua akimtaka achague upande wake wazi, akionya kuwa Mlima Kenya haupendi viongozi wasio na msimamo. Babu Owino amemfungulia mlango wa upinzani. Hata hivyo, Nyoro amechagua kubaki katikati, akisema bado ni mapema kuchukua msimamo kabla ya 2027. Wachambuzi wa siasa wanasema Nyoro ni mmoja wa viongozi wachache wenye ushawishi mkubwa Mlima Kenya. Kulingana na mchanganuzi wa siasa Stanley Wang’ombe, yeyote anayempata Nyoro atafaidika kisiasa. Nyoro, ambaye alichaguliwa mara mbili kwa kura nyingi Kiharu, alipata umaarufu akiwa miongoni mwa vijana waliomuunga mkono Ruto 2018. Hata hivyo, kimya chake katika baadhi ya matukio ya kisiasa kimeongeza presha kwake.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Talk of Town: Leader begs for attention on WhatsApp

The leader openly dismissed the strategy being pushed by the influential figure.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Why Fiolina and I are in love again!

I am forever grateful to God for giving me Fiolina.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Five health tests that could be the most meaningful Mother’s Day gift

Simple screenings can uncover hidden health risks early, making them one of the most meaningful...

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Want to be truly happy together? Create a strong emotional connection

You built that emotional link by spending time together while you were dating.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Oburu afichua mpango wa kufufua ODM huku akisema yu buheri wa afya

KIONGOZI wa chama cha ODM, Dkt Oburu Oginga, Mei 08, 2026 alijitokeza hadharani baada ya kutoweka kwa takriban wiki mbili na kuwahakikishia Wakenya kuwa yuko salama na mwenye afya njema. Kutoonekana kwake katika hafla muhimu za chama, ukiwemo mkutano mkubwa wa ODM uliofanyika Mombasa wiki iliyopita, kulizua uvumi kuwa alikuwa akiugua. Hata hivyo, Dkt Oginga alionekana jijini Kisumu akicheza gofu katika klabu ya Nyanza Golf Club, kuktana na marafiki pamoja na wafuasi wake kabla ya kuzungumza na wanahabari. Alisema alikuwa Nairobi akishughulikia masuala yake binafsi kabla ya kurejea Kisumu Alhamisi. “Sikutoweka. Sikukamatwa wala kuteswa. Niko salama, mwenye afya nzuri ” alisema Dkt Oginga. Aliwashukuru Wakenya kwa kujali hali yake na kusema kuwa aliamua kupumzika kwa muda mfupi huku akiwaachia viongozi wengine wa chama baadhi ya majukumu. “Huo ndio usimamizi bora. Huwezi kufanya kila kitu ilhali una viongozi uliowapa majukumu,” alisema. Alisema licha ya kutokuwepo kwake shughuli za ODM zimeendelea vizuri kutokana na chama hicho kuwa na mifumo madhubuti ya uongozi. Kiongozi huyo pia alifichua mipango ya chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027. Alisema ODM itaanza kufanya mikutano ya hadhara pamoja na mashauriano na makundi mbalimbali ya kijamii, hasa vijana. “Tutaandaa mikutano ya vijana, wanawake na watu wanaoishi na ulemavu ili kusikiliza maoni yao,” alisema. Kwa mujibu wa Dkt Oginga, shughuli hizo zitafikia kilele katika mkutano mkuu wa wajumbe wa chama (NDC), ambao utaamua mwelekeo wa ODM kuelekea uchaguzi wa 2027. “Ikiwa kutakuwa na muungano wa kisiasa, uamuzi huo utafanywa wakati wa NDC. Kama hakutakuwa na makubaliano, chama kinaweza kuamua kwenda uchaguzi kivyake,” alisema. Aliongeza kuwa kwa sasa ODM inalenga kujipanga na kuimarisha chama badala ya kushughulikia siasa za pembeni.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Mkutano mkubwa wa Afrika–Ufaransa Nairobi kuwaleta pamoja wajumbe 4,000

MKUTANO mkubwa wa Afrika na Ufaransa unaotarajiwa kufanyika Nairobi utawaleta pamoja zaidi ya wajumbe 4,000 wakiwemo marais 30, wafadhili wa kimataifa, viongozi wa biashara na mashirika ya kiraia. Huu utakuwa mkutano wa kwanza kama huo kufanyika katika nchi ya Afrika isiyozungumza Kifaransa, hatua inayotajwa kama ya kihistoria katika diplomasia ya kimataifa. Jana, polisi walitangaza kufungwa kwa barabara kuu na kuimarishwa kwa usalama jijini Nairobi kabla ya Mkutano huo. Barabara za City Hall Way, Parliament Road, Harambee Avenue na Taifa Road zitafungwa kwa umma kuanzia usiku wa Mei 11. Aidha, kutakuwa na msongamano wa muda katika Mombasa Road, Thika Road, Limuru Road na Kiambu Road misafara ya wageni ikisafiri kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) kwenda hoteli na eneo la mkutano. Kamanda wa Polisi Nairobi, Issa Mohamud, amesema mkutano huo utahudhuriwa na viongozi wakuu wa dunia. “Tutahakikisha wote wanaohudhuria wanalindwa ipasavyo. Tunawaomba Wakenya waendelee na shughuli zao na kushirikiana na maafisa wa usalama,” alisema. Alisema Polisi watafanya kazi kwa ushirikiano na Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF), Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS) na vikosi vya usalama vya Ufaransa na Umoja wa Mataifa. Mkutano huo unatarajiwa kuangazia masuala makuu yanayohusu mustakabali wa Afrika, yakiwemo mageuzi ya madeni na mfumo wa kifedha duniani, mabadiliko ya tabianchi, amani na usalama, pamoja na teknolojia na ubunifu. Kauli mbiu ya mkutano huo inaendana na ajenda za Rais William Ruto ambazo amekuwa akizisisitiza mara kwa mara katika majukwaa ya kimataifa. Miongoni mwa wageni wanaotarajiwa ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, Mahmoud Ali Youssouf, Mkurugenzi Mkuu wa IMF, Kristalina Georgieva, na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Sidi Ould Tah. Viongozi wa taasisi za Umoja wa Ulaya pamoja na mashirika mengine ya maendeleo pia wanatarajiwa kuhudhuria. Serikali ya Kenya inasema mkutano huu ni hatua muhimu ya kidiplomasia ambayo itaweka Kenya katikati ya mazungumzo ya kimataifa kuhusu mustakabali wa Afrika. Katibu wa Wizara ya Masuala ya Kigeni, Korir Sing’oei alisema mkutano huo unalenga kuanzisha uhusiano mpya kati ya Afrika na Ulaya unaojikita katika ushirikiano unaofaidi pande zote. “Tunashughulikia mazingira tofauti ya kidunia. Afrika na Ulaya zinapaswa kushirikiana kwa usawa na si kwa misingi ya kihistoria pekee,” alisema Sing’oei. Mjadala mkubwa utahusu biashara, uwekezaji, utengenezaji wa chanjo, mabadiliko ya tabianchi, usalama wa bahari na maendeleo ya teknolojia. Aidha, mkutano huo unalenga kuimarisha nafasi ya Afrika kama “bara la suluhisho” badala ya kutegemea misaada. Ufaransa, ambayo imekuwa ikikosolewa barani Afrika kuhusu mahusiano yake ya kihistoria na mataifa iliyotawala wakati wa ukoloni, inatarajiwa kutumia mkutano huu kuboresha taswira yake. Rais Emmanuel Macron anasemekana kuwa mstari wa mbele katika kuanzisha mwelekeo mpya wa ushirikiano huo.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Rigathi Gachagua’s DCP outshines UDA in Ol Kalou power play

Gachagua has effectively used the Ol Kalou by-election nominations to demonstrate that DCP is a...

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

WHO yaondoa wasiwasi kuhusu ugonjwa wa hantavirus unaohusishwa na panya

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) jana lilitangaza kuwa mlipuko wa virusi vya hantavirus una hatari ndogo duniani, likisema uwezekano wa maambukizi kusambaa kwa kiwango kikubwa au kusababisha athari kubwa za kiafya bado ni mdogo . Hadi sasa visa vinane vimeripotiwa, vikiwemo vifo vitatu. WHO imesema visa vitano vimethibitishwa kuwa vya hantavirus huku vingine vitatu vikichunguzwa. Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika, Dkt Mohamed Janabi, alisema mlipuko huo ni ukumbusho kuwa hata magonjwa nadra yanaweza kuyumbisha mifumo ya afya duniani kutokana na kuongezeka kwa safari na utangamano wa binadamu na wanyama. “Ingawa hatari bado ni ndogo, funzo ni wazi kuwa lazima tuwe tayari,” alisema Dkt Janabi. Aliwataka viongozi wa Afrika kuimarisha maandalizi na mifumo ya afya, akisisitiza umuhimu wa wahudumu wa afya wenye ujuzi. Mlipuko huo uliripotiwa kwa mara ya kwanza katika meli ya kitalii ya MV Hondius iliyokuwa ikisafiri kutoka Argentina kuelekea Antarctica na Bahari ya Atlantic Kusini ikiwa na watu 149 kutoka mataifa 23. Kisa cha kwanza kilishukiwa Aprili 6 baada ya mmoja wa abiria kuugua akiwa safarini. Siku tano baadaye, WHO ilithibitisha kifo cha kwanza. Virusi vya hantavirus hubebwa hasa na panya na huambukiza binadamu kupitia kinyesi, mkojo au mate ya panya. Maambukizi yanaweza kutokea mtu anapovuta hewa iliyochafuliwa. WHO imesema aina ya Andes ndiyo iliyobainika katika mlipuko wa sasa, na inaweza pia kusambazwa kutoka mtu mmoja hadi mwingine kupitia mawasiliano ya karibu ya muda mrefu. Dalili zake ni pamoja na homa, maumivu ya kichwa, misuli kuuma, maumivu ya tumbo, kichefuchefu na kutapika. Kwa sasa hakuna dawa maalum ya kutibu hantavirus, huku wagonjwa wakitibiwa kulingana na dalili zao. WHO imeweka watu 69 chini ya uangalizi barani Afrika baada ya kuhusishwa na visa hivyo. Nchini Kenya, Mkurugenzi Mkuu wa Afya, Patrick Amoth alisema hatari ya ugonjwa huo bado ni ndogo, lakini serikali imeimarisha uchunguzi katika viwanja vya ndege na bandari. Alisema hakuna kisa kilichoripotiwa nchini hadi sasa na kuwashauri waliotoka mataifa yaliyoathirika kufuatilia afya zao kwa wiki nane. Katibu wa Afya ya Umma, Mary Muthoni alisema Kenya inaendelea kufuatilia hali hiyo kwa karibu kupitia mifumo ya WHO na kanuni za kimataifa za afya.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Waziri wa Ardhi Kaunti ya Kajiado na afisa wadaiwa kukaidi amri ya mahakama

Waziri wa Ardhi Kaunti ya Kajiado, Hamilton Parseina, pamoja na afisa wa cheo cha chini katika idara hiyo wanakabili na hatari ya kifungo cha miezi sita jela au faini ya Sh200,000 kila mmoja kwa madai ya kukaidi amri ya mahakama kuhusu jaribio tata la kugawa kituo cha biashara cha Oloyiakalani katika Kaunti Ndogo ya Kajiado Magharibi . Mzozo huo umeibua vita vikali vya kisheria kati ya wakazi na Serikali ya Kaunti ya Kajiado, huku wakazi wakidai maafisa wa kaunti walilenga kinyume cha sheria eneo hilo la ekari 68 bila kufuata utaratibu unaotakiwa. Kaunti hiyo ilianza kwa kuwasilisha wazo hilo kupitia zoezi la ushirikishaji wa umma, ambalo lilipingwa na wakazi, hali iliyowasukuma kuwasilisha kesi katika Mahakama ya Hakimu Kajiado kupitia kesi nambari MCCCMISC/E032/2026 kwa Notisi ya Hoja ya Machi 30, 2026 mbele ya Hakimu Mkuu Roseline Oganyo. Kupitia kwa wakili Enock Nyongesa, walalamishi Ronald Kiranti, Solomon Kikanae na Obadiah Likam, kwa niaba yao na wakazi wengine, waliomba mahakama izuie washtakiwa, wakiwemo Waziri wa Ardhi wa Kaunti Ardhi Hamilton Parseina, Afisa Mkuu katika Idara ya Ardhi, Idara ya Mipango na Maendeleo ya Miji, Serikali ya Kaunti ya Kajiado pamoja na Tume ya Kitaifa ya Ardhi (NLC), kuendelea na zoezi hilo hadi kesi itakaposikizwa na kuamuliwa. Walalamishi walieleza mahakama kuwa tarehe zilizotajwa katika notisi zilikuwa tayari zimepita kwani zoezi hilo lilikuwa limepangwa kufanyika Jumanne, Machi 17, 2026. Walidai kuwa Serikali ya Kaunti au mamlaka husika ilipaswa kuandaa notisi mpya inayotoa muda wa kisheria wa siku 21 kabla ya kuanza kwa zoezi hilo. Aidha, waliambia mahakama kuwa notisi iliyotolewa haikukidhi masharti ya kikatiba kuhusu ushirikishaji wa umma, ambayo yanataka matangazo hayo kuchapishwa katika magazeti yenye usambazaji mkubwa. Waliongeza kuwa ardhi inayozungumziwa ni ardhi ya umma inayosimamiwa na Tume ya Kitaifa ya Ardhi na haijawahi kutengwa wala kupangwa na iliyokuwa Halmashauri ya Kaunti ya Olkejuado. Kwa hivyo, walisema jukumu la kusimamia ardhi ya umma kwa niaba ya serikali za kaunti na kitaifa ni la Tume ya Kitaifa ya Ardhi wala si Ofisi ya Afisa Mkuu. Kupitia kwa hati ya kiapo, walalamishi pia walidai kuwa jamii haikuwahi kuomba upangaji wa mji huo kupitia mkutano wa umma wala ombi la maandishi. Waliitaka Serikali ya Kaunti kuahirisha zoezi hilo ili jamii ipate muda wa kutosha kujadili huduma za umma zinazopaswa kuhifadhiwa kwenye ardhi hiyo. Wakazi hao pia walidai kuwa ardhi hiyo inapakana na mashamba binafsi na kwamba migogoro ya mipaka inapaswa kwanza kushughulikiwa na Msajili wa Ardhi kabla ya mchakato wowote wa upangaji kuanza ili kuepuka matatizo ya kisheria na uvamizi wa mashamba ya watu binafsi. Aidha, walieleza kuwa maeneo hayo kwa sasa hayana maendeleo yoyote yanayohitaji upangaji wa haraka na kwamba mchakato wowote unapaswa kufanywa kwa utaratibu unaofaa na kwa mashauriano na Tume ya Kitaifa ya Ardhi pamoja na jamii ya eneo hilo. Mnamo Machi 30, 2026, mahakama ilitoa amri ya muda kuwazuia washtakiwa, maajenti wao au wawakilishi wao kuendesha au kuendelea na zoezi lolote la ushirikishaji wa umma, upangaji, ugawaji au utoaji wa ardhi katika Kituo cha Biashara cha Oloyiakalani hadi kesi hiyo isikizwe na kuamuliwa. Kesi hiyo itatajwa tena Mei 26, 2026 mbele ya Hakimu Mkuu Roseline Oganyo. “Fahamuni kwamba kutotii au kutofuata amri hii ya mahakama kutasababisha hatua za kisheria dhidi yenu na mtu mwingine yeyote atakayekaidi amri hiyo,” ilisema sehemu ya amri ya mahakama. Hata hivyo, wakili wa walalamishi alidai kuwa maahenti wa washtakiwa walionekana mapema wiki hii mjini humo wakijaribu kuendeleza zoezi hilo lililozuiwa, hatua aliyosema ilisababisha taharuki miongoni mwa wakazi na ni dharau kwa mahakama inayoweza kufanya waadhibiwe kisheria. Mtu anayepatikana na hatia ya kuidharau mahakama anaweza kutozwa faini isiyozidi Sh200,000, kufungwa jela kwa muda usiozidi miezi sita au kupewa adhabu zote mbili.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Mums, what nickname has your teenager given you in their phone contacts?

One woman said that her children had saved her number under the name 'Fire si Fire'.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Kinyanjui ashangaza seneti akisema mama mboga na mahasla ndio walitaka viwanda katika kaunti

WAZIRI wa Biashara, Lee Kinyanjui, amefichua kuwa mpango wa serikali wa kujenga viwanda kwenye kaunti kwa thamani ya Sh23.5 bilioni ulianzishwa bila utafiti kufanywa. Akizungumza mbele ya Seneti Jumatano, Bw Kinyanjui alisema mpango huo ulitokana na mazungumzo aliyokuwa nayo Rais William Ruto na makundi ya “mama mboga” na “mahasla” wakati wa kuandaa manifesto ya Kenya Kwanza kabla ya uchaguzi wa 2022. Waziri huyo alisema maoni yaliyotolewa na wananchi wakati wa kampeni yalitosha kuchukuliwa kama ushirikishaji wa umma kuhusu miradi waliyoitaka. “Wakati mwingine tunajificha nyuma ya maneno makubwa kama tafiti za ufaafu ilhali tayari tunajua wananchi wanahitaji nini,” alisema. Alilinganisha hali hiyo na mpango wa elimu ya bure ulioanzishwa na Rais wa tatu wa Kenya Mwai Kibaki bila utafiti maalum lakini ukafaulu. Kauli hiyo imeibua mjadala mkali huku maseneta wakionya kuwa baadhi ya maeneo hayo ya viwanda huenda yakageuka miradi hewa isiyo na manufaa kwa wananchi. Seneta wa Kitui, Enock Wambua alisema ilikuwa kosa kuweka gharama sawa kwa kaunti zote 47 bila kuzingatia tofauti za maeneo. Kila kaunti ilitakiwa kutoa Sh250 milioni huku serikali kuu ikitoa kiwango sawa, jumla ikiwa Sh500 milioni kwa kila mradi. Hata hivyo, magavana wamekiri kuwa gharama imeongezeka katika baadhi ya maeneo. Gavana wa Nyeri, Mutahi Kahiga alisema mradi katika kaunti yake sasa utagharimu Sh589 milioni badala ya Sh500 milioni zilizopangwa awali. Seneta wa Busia, Okiya Omtatah alisema hakuna hata kaunti moja yenye utafiti wa kisayansi unaoonyesha miradi hiyo inawezekana au itakuwa na manufaa. Aidha, baadhi ya wakandarasi wameacha kazi huku miradi ikikwama. Kati ya miradi 17 iliyoanzishwa mwaka 2023, ni mitano pekee iliyo tayari kuzinduliwa, kulingana na Waziri Kinyanjui. Ripoti ya Afisi ya Bajeti ya Bunge pia inaonyesha baadhi ya kaunti ziko chini ya asilimia 30 ya utekelezaji huku miradi ikikwama kabisa katika kaunti 13. Licha ya changamoto hizo, serikali inasema mpango huo ulikusudiwa kuongeza thamani ya mazao, kupunguza hasara baada ya mavuno na kuzalisha nafasi za ajira kwa vijana. na wafanyabiashara wadogo.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

2027: Mirengo mitano yang’ang’ania kura za Mlima Kenya

VITA vikali vya kisiasa vya kudhibiti kura za eneo la Mlima Kenya Mashariki vimeibuka huku makundi matano ya kisiasa yakijipanga kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027. Makundi hayo yanawaunganisha Naibu Rais Kithure Kindiki, kinara wa chama cha Democracy for Citizens Party (DCP) Rigathi Gachagua, mwanasiasa Fred Matiang’i wa Jubilee, Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru na aliyekuwa Gavana wa Meru Kawira Mwangaza. Mlima Kenya Mashariki unajumuisha kaunti ya Meru iliyo na wapiga kura 772,000, Tharaka Nithi 232,000 na Embu 334,000. Washirika wa Profesa Kindiki sasa wanataka pia Kirinyaga yenye wapiga kura 376,000 ijiunge na muungano huo. Kwa mujibu wa takwimu za IEBC za 2022, eneo hilo lina takriban wapiga kura milioni 1.7, idadi inayotarajiwa kuongezeka hadi milioni 2.5 kufikia 2027. Waziri wa Utumishi wa Umma Geoffrey Ruku, amesema mpango huo unalenga kupambana na kutengwa kisiasa kwa eneo hilo na pia kuwapa wakazi wa Mashariki nguvu ya kujadiliana kisiasa bila kutegemea Mlima Kenya Magharibi. “Kama Gachagua ataonekana kuwa na nguvu zaidi kisiasa, sisi wa Mashariki hatutamfuata. Tutabaki Mashariki chini ya uongozi wa Kindiki,” alisema Ruku. Mpango huo unaungwa mkono na Gavana wa Embu Cecily Mbarire ambaye pia ni mwenyekiti wa chama tawala cha UDA. Hata hivyo, wachambuzi wa siasa wanaonya kuwa mkakati huo unaweza kumdhoofisha Profesa Kindiki kitaifa kwa kumfanya aonekane kama kiongozi wa eneo dogo badala ya mwanasiasa wa kitaifa. Changamoto kubwa kwa Kindiki ni kwamba viongozi wengine ndani ya serikali jumuishi kutoka Pwani, Magharibi na Nyanza pia wanapigania kuwa mgombea mwenza wa Rais William Ruto mwaka 2027. Kwa upande mwingine, Gachagua anaonekana kuwa na ushawishi mkubwa katika eneo pana la Mlima Kenya linalojumuisha Kiambu, Murang’a, Nyandarua, Nyeri na Laikipia, maeneo yenye zaidi ya wapiga kura milioni tatu. Katika Mlima Kenya Mashariki, kundi la Gachagua linategemea Mithika Linturi Meru, Kamau Murango Kirinyaga na Mbunge wa Manyatta Gitonga Mukunji Embu. Kawira Mwangaza pia ameibuka tena kisiasa baada ya kuondolewa mamlakani mwaka 2024, kupitia chama chake cha Umoja na Maendeleo Party. Ameungana na kundi la Linda Mwananchi ndani ya ODM linalohusisha Seneta Edwin Sifuna na Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino. Kwa upande wake, Fred Matiang’i amejiunga na aliyekuwa Gavana wa Meru Peter Munya katika kuimarisha ushawishi wake eneo hilo. Anne Waiguru naye ameonekana kupigana kivyake huku akionyesha nia ya kuwa mgombea mwenza wa Rais Ruto mwaka 2027. Gachagua amesema mipango hiyo yote inalenga kugawa kura za Mlima Kenya ili eneo hilo lisipige kura kwa pamoja dhidi ya Rais Ruto. “Hii si vita kati ya Mashariki na Magharibi. Serikali ndiyo inafadhili mgawanyiko huu. Lazima nguvu zote zinazompinga Ruto ziungane nyuma ya mgombea mmoja wa upinzani,” alisema Gachagua akiwa Kajiado wiki iliyopita. Mchanganuzi wa siasa John Okumu anasema kati ya makundi hayo matano, mawili pekee yanaunga mkono kuchaguliwa tena kwa Rais Ruto. Anasema viongozi wanaoonekana kuwa na nguvu kubwa zaidi kwa sasa ni Kindiki, Gachagua na Kawira Mwangaza. “Kindiki ana nafasi kubwa kwa kuwa Naibu Rais lakini anaonekana kuogopa kuunganisha Mlima Kenya kama ngome moja. Gachagua anaonekana kuwa mbele kisiasa huku Mwangaza akijaribu kupanua ushawishi wake nje ya Mashariki,” alisema Okumu. Mchanganuzi mwingine, Malila Munywoki, amesema vita vya Mlima Kenya Mashariki vinaweza kuwa hatari zaidi kwa Rais Ruto kwa sababu wengi wa viongozi huko wanapinga kuchaguliwa kwake tena. “Ukichunguza Gachagua, Matiang’i na Mwangaza, wote wanampinga Ruto. Hilo linaonyesha kuwa Rais anaweza kupata wakati mgumu sana 2027, na Kindiki ndiye atakayepata pigo la kwanza,” alisema Munywoki.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Africa’s richest man Aliko Dangote eyes Kenya for new refinery

Dangote is looking at Kenya as the site of a 650,000-barrel-a-day oil refinery.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Allan Thigo, Harambee Stars and Gor Mahia icon, passes away

Thigo was a rare "player-cum-coach" who dominated the pitch for 12 seasons.

10 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Mauaji ya akina mama yazidi nchini huku tukiadhimisha Siku ya Akina Mama duniani

VISA vya mauaji ya wanawake na wasichana nchini Kenya vinaendelea kushtua taifa, kila kisa kikiwa na maumivu mapya na maswali mazito kuhusu usalama wa wanawake katika jamii. Kutoka mashambani hadi mijini, kutoka Pwani hadi Bonde la Ufa, visa hivi vinaonyesha mtindo unaozidi kuongezeka wa ukatili unaohusishwa na mapenzi yaliyovunjika, migogoro ya kifamilia na hasira zisizodhibitiwa. Katika Kaunti ya Bomet, Ivine Cheche Chepkoech, msichana wa miaka 17, aliuawa kikatili akiwa nyumbani kwa nyanya yake. Alikuwa akiandaa chakula cha jioni kabla ya kushambuliwa kwa kitu kizito kichwani na baadaye kukatwa kwa kitu chenye ncha kali. Mwili wake baadaye ulipatikana ukiwa umetupwa katika shamba la chai. Polisi wanamshuku mpenzi wake wa zamani kuwa mhusika wa shambulio hilo. Katika Kaunti ya Nakuru, mauaji ya wanawake yamechukua sura ya kutisha zaidi. Mwanamke mmoja, Annita Mugweru, aliuawa kwa kudungwa kisu akiwa nyumbani kwake kufuatia mzozo wa kifamilia, tukio lililotokea mbele ya mtoto wake mdogo. Katika tukio jingine, mlinzi, Jackline Awuor, alipatikana ameuawa na kichwa kukatwa katika eneo la Bahati, baada ya kutoweka kazini, huku mpenzi wake akihusishwa na mauaji hayo. Huko Siaya, kijana wa miaka 21, Rose Benta Apondi, alipatikana akiwa ameuawa baada ya kutoweka kwa wiki mbili. Familia yake ilieleza kuwa alikuwa akipokea vitisho kutoka kwa mpenzi wake wa zamani baada ya kuvunja uhusiano. Mwili wake ulikuwa umeharibika vibaya kiasi cha kufanya uchunguzi wa kifo kuwa mgumu. Katika eneo la Meru, mwanafunzi Diana Cherono, miaka 20, alipatikana ameuawa na mwili wake kutupwa kwenye bomba la maji taka wiki kadhaa baada ya familia yake kumtafuta bila mafanikio. Tukio hilo liliwaacha wazazi wake wakiwa na majonzi makubwa baada ya kugundua kuwa binti yao alikuwa tayari ameuawa mbali na nyumbani. Katika Bonde la Ufa, mkasa mwingine uliogusa hisia ni wa familia ya Elgeyo Marakwet, ambapo mwanamume alimuua mke wake na watoto wake wawili kutokana na mgogoro wa kifamilia. Katika kaunti ya Baringo, mwanamume mwingine alimuua mkunga akimlaumu kwa kifo cha mtoto wake mchanga. Mshukiwa alitumia mshale wenye sumu. Pwani nayo haijaachwa nyuma. Katika kaunti za Mombasa na Kilifi, visa vya wanawake na watoto kuuawa kikatili vimeongezeka. Mwanamke mjamzito alipatikana ameuawa na mwili wake kutupwa ndani ya jengo ambalo halijakamilika. Mtoto wa miaka minane naye alipatikana ameuawa baada ya kupote na kuzua hasira na hofu katika jamii. Katika tukio lingine la kushtua zaidi, msichana wa miaka 11 aliuawa baada ya kubakwa, kisha mwili wake kuwekwa kwenye mfuko na kuachwa kando ya njia. Polisi wanasema uchunguzi unaendelea, lakini jamii imebaki ikitaka majibu na hatua kali zaidi. Visa hivi vinaonyesha janga la kitaifa la ukatili dhidi ya wanawake, ambalo limekuwa likihusishwa zaidi na watu wa karibu—wapenzi, waume, na hata wanafamilia. Hali hii imeibua hofu kuwa nyumbani, ambako kunapaswa kuwa mahali salama, kumekuwa hatari kwa wanawake na watoto. Wataalamu wa masuala ya kijamii wanasema chanzo kikuu ni mchanganyiko wa migogoro ya mapenzi, ukosefu wa mawasiliano, na matatizo ya afya ya akili yasiyotibiwa. Wanasema pia kwamba baadhi ya wahusika hushindwa kudhibiti hasira zao, na hivyo kugeukia ukatili wa hali ya juu. “Tunashuhudia jamii inayokosa njia za amani za kutatua migogoro,” anasema mtaalamu mmoja wa ushauri nasaha Faith Queen Chebet,, akiongeza kuwa mazungumzo ya mapema yanaweza kuzuia visa vingi vya mauaji. Wadau wa haki za wanawake wanaitaka serikali kuchukua hatua kali zaidi, ikiwemo kuongeza ulinzi, kuimarisha mifumo ya kuripoti vitisho na kuharakisha mashauri ya mauaji mahakamani. Wanasema kuchelewa kwa haki kunachochea wahalifu kuendelea na ukatili huu. Hata hivyo, familia nyingi zimebaki zikilia, zikikosa majibu na faraja. Kila kisa kinachotokea kinaacha pengo jipya, na kila kifo kinaongeza presha kwa taifa kuchukua hatua za haraka kabla hali haijazidi kuwa mbaya zaidi. Kwa sasa, swali kubwa linalobaki mdomoni mwa Wakenya ni moja: nani anaua wanawake hawa, na kwa nini damu yao inaendelea kumwagika bila kukoma?

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Sammy Ngotho crushes the competition to clinch the DCP ticket for Ol Kalou

With 12,957 votes, Ngotho demonstrated significant local support.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Motherhood unfiltered: The women turning social media into support networks

A growing number of mothers are turning their parenting journeys into digital platforms that...

10 May 2026

Daily Nation Kenya

West Pokot gold mine: How locals ignored early warnings before deaths of 15

County commissioner says most of those who died have already been buried/.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

All hail mothers: Here is what motherhood means to us

From younger mums to older mums, the constant was that the bond never fades, even though the...

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Inside Africa- France summit: What countries want from Nairobi talks

Some 39 African countries will participate at the summit.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Super mums: Mothers successfully juggle sporting careers with raising family

They strike a fine balance between demands of professional sport and raising children.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

How mama mboga, hustlers drove stalled Sh23bn county jobs plan

Sh23 billion industrial parks programme was started without proper feasibility studies.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Ruto, Macron Nairobi summit plan and why France is courting Africa

For France, the meeting may be an opportunity to mend its image.

10 May 2026

Daily Nation Kenya

Is Kenya truly protecting the dignity of mothers and newborns?

10 May 2026

Daily Nation Kenya

2027 elections and politics of Kamikaze

The political ground is moving quietly beneath our feet.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Why Senator Nyamu must step down immediately

Senator Nyamu has proven she lacks the sobriety required to lead.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Kenya is a country of minorities

No African country is a racial or ethnic monolith.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Curb illegal mining deaths

Rescue teams searched through the debris amid fears that more people may have been trapped inside.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Address concerns over digital school fees plan

Critics have accused the government of ignoring the serious challenges facing parents and schools.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Five titles in a row! Kabras Sugar beat KCB to win Kenya Cup

Kabras become only the third team in history of Kenyan rugby to win league crown five...

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Ruto touts Sh200bn growth in education budget since 2022

This figure is expected to rise further to Sh767 billion in the 2026/27 financial year, he says.

9 May 2026

Taifa Leo (Swahili)

Wito serikali ihakikishe watoto wote wanapata elimu bila ubaguzi

KINARA wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, ameihimiza serikali kuhakikisha kila mtoto nchini anapata elimu bila vikwazo, akisema wanafunzi wengi kutoka familia maskini wanatatizika kuendelea na masomo kutokana na ukosefu wa karo na ufadhili wa kutosha. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Lizah Foundation International jijini Nairobi, Kalonzo alisema elimu ni haki ya msingi ambayo serikali inafaa kuipa kipaumbele ili kusaidia watoto kufikia ndoto zao. “Ni jambo la kuhuzunisha kuona wanafunzi wengi wakikosa kuendelea na masomo kwa sababu ya changamoto za kifedha. Serikali inapaswa kutenga rasilimali za kutosha katika elimu. Ninaona roho ya Wangari Maathai ndani ya Lizah, na naamini taasisi hii itafika mbali katika kusaidia wasiojiweza,” alisema Kalonzo. Waziri wa Kawi, Opiyo Wandayi, alisema serikali ya Kenya Kwanza itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kwa usawa kote nchini bila ubaguzi wa kikabila au kisiasa. “Nchi hii ni ya Wakenya wote, na maendeleo yatagawanywa kwa usawa katika maeneo yote,” alisema Wandayi. Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Ouma Oluga, alisema wizara hiyo itashirikiana na taasisi hiyo kuhamasisha jamii kuhusu masuala ya afya na ustawi. Lizah Foundation International, inayoongozwa na mwanahabari mkongwe Lizah Mutuku, imekuwa mstari wa mbele kusaidia miradi ya mazingira, elimu kwa watoto wanaotoka katika familia maskini na kuwawezesha wasichana kufanya maamuzi bora maishani. Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Ezekiel Mutua, wabunge, wanahabari na viongozi mbalimbali wa kijamii.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Write more books, CJ Koome urges judicial officials

The Judiciary becomes more accessible to the public, through books and public conversations...

9 May 2026

Daily Nation Kenya

State plans Sh360bn housing blitz after 2027 polls

The government anticipates significant revenue from houses currently under construction.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Photographic memory? Sorry, it’s a myth

Human memory does not work like a recording device.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Police announce closure of key roads as Nairobi hosts France-Africa Summit

More than 30 heads of state and up to 4,000 delegates are expected to attend the summit.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Kabras Rugby team captain optimistic ahead of KCB clash in Kenya Cup final

9 May 2026

Daily Nation Kenya

Six killed after gunman opens fire on matatu in Mandera in suspected terrorist attack

They were travelling from Mandera town to Arabia township near the Kenyan-Somali border.

9 May 2026

Daily Nation Kenya

‘I have a right to be forgotten’: Tycoon Mary Wambui sues Google on past Sh2.2bn tax case

She argues that the case against her was withdrawn but years later, the negative articles are...

9 May 2026